Saturday 26 March 2016

USIUE NDOTO YAKO KWASABABU YA PESA



USIUE NDOTO  YAKO  KWASABABU YA PESA

Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Kila mtu duniani ana ndoto haijalishi ni ndoto gani unayo ,ndoto uliyonayo ina thamani kubwa kuliko fedha kuliko kitu chochote kile,Ndoto uliyonayo ina nguvu kubwa ya kubadilisha maisha yako na kukufikisha sehemu ambayo ulitaka ufike ama zaidi ya pale ulipotarajia kufika.

Ndoto yako inaweza kukupeleka sehemu mbalimbali duniani ukazunguka kufanya mambo yako si kwa

Saturday 21 November 2015

FURSA UNAZOWEZA KUTENGENEZEA KIZAZI CHAKO KWA WEMA UNAOUTENDA LEO



FURSA UNAZOWEZA KUTENGENEZEA KIZAZI CHAKO KWA WEMA UNAOUTENDA LEO

Na Samuel Sasali

Wema Ni Akiba, Wema Hauozi... Mara nyingi sana ni rahisi kumfanyia wema yule ambaye amekufanyia wema ama una amini anaweza kukufanyia wema hapo baadae. Ni nadra sana kutenda wema kwa mtu aliyewahi kukutendea uovu ama ubaya ama ambaye unaamini atakufanyia ndivyo sivyo.

JUA UWEZO ULIONAO ILI UFANIKIWE



JUA UWEZO ULIONAO ILI UFANIKIWE


Na Samuel Sasali


Usikomalie kufanya jambo ambalo hujapewa neema ya kufanya utabaki unapoteza muda, unapoteza nguvu na unapoteza hata mvuto kwa kung’ang’ania kufanya. Kuna watu nimewahi ona waliwahi ng’ang’aniza kufanya mambo ya kakwama, lakini kazi ile ile akaja akafanya mtu mwingine kwa wepesi sana mpaka watu wakauliza “ulikuwa wapi saa zote”?. 

Friday 16 October 2015

JINSI YA KUTENGENEZA MTAZAMO CHANYA UTAKAOKUFIKISHA KWENYE MAFANIKIO




JINSI YA KUTENGENEZA MTAZAMO CHANYA  UTAKAOKUFIKISHA KWENYE MAFANIKIO

Na Ferdinand Shayo














Mafanikio haimaanishi kukosekana kwa kushindwa bali ni kushinda vita ila sio kwa kila pambano.Katika maisha ya kila siku unaweza ukawa umeshakutana ama kuwaona watu wanaoshangaa maisha yao,wanashangaa kwasababu walikubali majaliwa 

Thursday 15 October 2015

ACHA KUOTA NDOTO TIMIZA NDOTO ZAKO



ACHA KUOTA NDOTO TIMIZA NDOTO ZAKO

Na  Samuel Sasali


Kati ya changamoto kubwa tulizonazo kwenye kizazi chetu ni kuamua kufanya na kusimamia kile unachoamua kufanya.

Misukosuko ndiyo chachu ya maendeleo ya ndoto zetu.



Misukosuko ndiyo chachu ya maendeleo ya ndoto zetu.

Na Samuel Sasali

Ukweli ni kwamba Viwanja vya ndege kuna mazingira mazuri kuliko angani lakini ndege hazijaumbwa zikae airport, kinachotofautisha gari na ndege ni anga.

 Angani kuna misukosuko lakini ndoio ndege zimetengenezewa mazingira thabiti. Hata kama Bandarini ni pazuri namna gani lakini ukweli ni kwamba Meli na Boti zimeumbiwa majini.

Hapo ulipo inawezekana ni kiwanja cha ndege ama bandarini ambapo kiukweli ni pazuri sababu hapana misukosuko lakini kumbuka ili ndege itoke destination moja kwenda nyingine kuna dhoruba kadhaa itakumbana nazo.

Thursday 8 October 2015

NIDHAMU YA FEDHA NGUZO YA MAFANIKIO YA KIUCHUMI



NIDHAMU YA FEDHA NGUZO YA MAFANIKIO YA KIUCHUMI

Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Ili kuyafikia mafanikio ya uchumi nidhamu ya fedha ni ngazi inayoweza kukupandisha juu katika kiwango kingine cha mafanikio na kuyafikia malengo  uliyojiwekea.

Saturday 3 October 2015

Badili maisha kupitia fikra zako

by Robison Sisyan | Makala

 
WATAALAMU wa masuala ya saikologia wanasema zaidi ya asilimia 95 ya maisha yetu ni matokeo ya fikra zilizopo ndani yetu na asilimia 5 ni mazingira yanayotunguka na vitu vingine.

Thursday 1 October 2015

TUNAWAANDAAJE WATOTO WANAPOFIKIA UMRI WA KUBALEHE

TUNAWAANDAAJE WATOTO WANAPOFIKIA UMRI WA KUBALEHE
Na Ferdinand Shayo,Arusha.
 
Wazazi wengi wamekua wakikaa kimya na kuona aibu kuzungumza na watoto wao juu ya mabadiliko ya miili yao inayotokea pindi wanapobalehe na namna ya kuweza kukabiliana na mabadiliko hayo kabla ya kuingia kwenye hatari.

TAFUTA VITU VISIVYOONEKANA ILI UFANIKIWE

TAFUTA VITU VISIVYOONEKANA ILI UFANIKIWE

Na Ferdinand Shayo



Watu wengi huvutiwa na kupenda vitu vinavyoonekana kwa macho lakini wamesahau kuwa kuna vitu visivyoonekana kwa urahisi na vina thamani kubwa kuliko vile vinavyoonekana kwa urahisi mfano wa madini ya dhahabu ama Tanzanite.
Usiuchekee Uamuzi Utakaokugharimu Baadae.

Na Samuel Sasali

Ugumu ama wepesi wa maamuzi hutegemea sana uwezo wa muamuaji katika jambo lililo mbele yake. Na ugumu ama wepesi haupimwi kijinsia wala kiumri wala kinamna yoyote ila kwa uwezo ambao kila mtu amejaaliwa na Mungu.

Tuko hiVi tuliVyo kutokana na maamuzi mbalimbali ambayo tuliwahi kuamua. Nyumba unayoishi, biashara unayofanya kila uliCho naCho ni matokeo ya maamuzi uliyowahi amua wakati fulani kwenye maisha. Kuna maamuzi ambayo wakati mwingine tumekuwa tukiamua huku tukijua fika maamuzi hayo yatatugharimu lakini pengine tumeamua kufanya tukijiaminisha kuwa mabaya yanaweza yasitokee.