Thursday 15 October 2015

ACHA KUOTA NDOTO TIMIZA NDOTO ZAKO



ACHA KUOTA NDOTO TIMIZA NDOTO ZAKO

Na  Samuel Sasali


Kati ya changamoto kubwa tulizonazo kwenye kizazi chetu ni kuamua kufanya na kusimamia kile unachoamua kufanya.


Wengi wetu ni kweli tuna ndoto na wengine wana ndoto kubwa sana. Wengi wetu tuna mikakati mingikila siku tunasema "wacha nijipange, wiki ijayo naanza"....mwingine anaapa na kuapa kuwa mwezi ujao anaanza rasmi lakini wapi mambo yale yale unadhani kwamba hataki kutimiza ndoto la hasha sababu anayo uwezo anao unadhani kinakosekana nini?NIA ndiyo inayokosekana katika kutimiza ndoto zetu.

Nia ya kutenda na kutimiza ndoto inahitaji nidhamu ya hali ya juu kuweza kutimizwa. Muulize mtu yeyote ambaye ambaye alitimiza ndoto bila kuwa na nidhamu.

Nia haipimwi kwa mikakati ila inapimwa kwa utekelezaji. Wengi wetu tuna Diarly za kuandikia tuna mikakati ya kimaandishi lakini Utashi wa kutimiza matakwa na mikakati na Nidhamu ya kutimiza ndoto ndiyo changamoto kubwa.

Dhamira ya utekelezaji ikiwa chini kuliko mihemko ya kutaka kuonekana na watu kuwa nawe una ndoto ya kutimiza hupelekea kubaki vile vile katika maisha yako.

Ni lazima utengeneze mazingira ya kuinua nia yako ya ndani kwa njia mbalimbali. Inua nia yako ya kutimiza ndoto kwa kuuliza watu, kusoma vitabu, kama unaamini katika Mungu fanya maombi, watembelee wanaotimiza ndoto kama ya kwako, tafuta taarifa za kutosha kuhusiana na ndoto yako.






No comments:

Post a Comment