Friday 16 October 2015

JINSI YA KUTENGENEZA MTAZAMO CHANYA UTAKAOKUFIKISHA KWENYE MAFANIKIO




JINSI YA KUTENGENEZA MTAZAMO CHANYA  UTAKAOKUFIKISHA KWENYE MAFANIKIO

Na Ferdinand Shayo














Mafanikio haimaanishi kukosekana kwa kushindwa bali ni kushinda vita ila sio kwa kila pambano.Katika maisha ya kila siku unaweza ukawa umeshakutana ama kuwaona watu wanaoshangaa maisha yao,wanashangaa kwasababu walikubali majaliwa 

yalipowapeleka.Wachache sana wanaofanikiwa kwa majaliwa lakini wengi wanapata shida kwenye maisha kwasababu ya hili.

Kwanza kabisa tengeneza ama panga vitu vifuatavyo (Action plan) inayojikita kwenye mambo makuu matatu:1.Nini hasa unataka kukifikia (lengo) 2.Na unahitaji lengo lako litimie lini? 3.Unafikiri utalifikiaje hilo lengo unaangalia mikakati uliyoiweka,njia utakazotumia kufikia lengo lako,mbinu na vifaa ili kuweza kufanikisha malengo yako katika maisha.

Suala la Mafanikio katika maisha linaanzia kwenye mitazamo na fikra zilizoko ndani ya mtu,kile kilichoko ndani ya mtu ndicho kitakachomhesabia mafanikio yake.Mtizamo peke yake ndo msingi wa maisha ambapo mtizamo unachukua asilimia 64 ya nafasi katika maisha ya mtu.Ni vyema tukajifunza kutengeneza mitazamo chanya ili tuweze kufanikiwa na njia mojawapo ya kutengeneza ni kufikiria mema tu na kuacha kufikiria mabaya kwasababu siri ya kushinda katika maisha ni kuondoa fikra za kushindwa.

Mfano mtu mmoja alikuwa akiishi kwa kuuza mapulizo.Alifanya baishara yake hiyo kwa muda mrefu, na kupata mafanikio mazuri sana hasa kiuchumi. Baada ya watu wengi kuzuka waliofanya biashara kama yakwake, uchumi wake ukaanza kupormoka siku hadi siku. Baada ya kuona hali hiyo akaamua kutafuta ufumbuzi wa tatizo lake.

 Ndipo akakutana na mwanasayansi aliyefanya kazi katika maabara moja hapo mjini.Mwanasayansi huyu akampa mbinu ya kuyajaza maputo yale kwa hewa(Hydrogen) ambayo ni nyepesi kuliko hewa hii ya kawaida(Oxygen) tuivutayo katika miili yetu.

Mfanyabiashara yule akafanya kama alivyo shauriwa na mwanasayansi, kuyajaza maputo hewa ya hydrogen, kwa maana hiyo yakawa.
 

Umewahi kujiuliza kwanini watu,au kampuni,nchi nyingine zina mafanikio kuliko nyingine? hii siyo siri,hawa watu wanafikiri na kufanya kazi vizuri,wamejifunza jinsi ya kuwekeza kwa watu wenye mitazamo chanya.

Mafanikio ya mtu,kampuni au nchi yanategemea sana ubora wa watu wake­.Hivyo umeona kuwa ni jinsi gani mtazamo ni msingi wa mafanikio.

Mfano kuna jengo moja huko Marekani lenye urefu wa mita 190.8,lia uzito wa tani 10,884.Ambapo tani 6,349 iko chini ya ardhi ambayo ni sawa na asilimia 60% ya jengo zima.Hii ina maanisha na kuoyesha kwamba majengo marefu duniani yana misingi imara hata karibia robo tatu ya jengo zima.


Kama iliyo kwa jengo refu na zuri duniani lilivyo na msingi imara,vivyo hivyo hata wewe unapaswa kuwa na msingi imara.Na huo msingi imara kwa kila binadamu ni MTIZAMO.


Yuko mkulima mmoja wa Afrika alikuwa na shamba kubwa analilima na bado alikuwa na maisha duni siku moja akaja mtu mwenye busara nyumbani kwake akamuambia kuwa iwapo mkulima huyo angepata almasi yenye ukubwa sawa na kichwa chake angekuwa tajiri wa kutupwa mpaka kufa kwake yeye na watoto wake pamoja na wajukuu.

Mkulima huyo aliposikia hivyo haikupita muda akauza shamba lake lote akasafiri kwenda nchi za nje yeye na familia yake kwenda kuitafuta almasi na kuinunua alipofika huko akakuta pesa aliyokuwa nayo ni ndogo haiwezi kununua almasi na alishaitumia kama nusu hivi kwa gharama za kusafiria mtu huyo kwa presha na mawazo akaamua kujinyonga akaona kuwa hapo alipofika hawezi kusonga mbele wala kurudi nyuma shamba na nyumba alishaviuza.

Baada ya muda mfupi yule mtu aliyeuziwa lile shamba akagundua kuwa kwenye shamba lile kulikuwa na mawe yanayong`aa akayachukua kwenda kupima akakuta ni almasi akayauza na kuwa tajiri,yule mtu mwenye busara aliposikia habari hizo akaamua kwenda kumtembelea yule mkulima alipofika kwenye lile shamba akamuulizia akaambiwa kuwa mkulima huyo alishaliuza shamba hilo kwa mtu mingine na akasafiri kuelekea mbali,yule mtu mwenye busara akasikitika sana.

Stori hii ya mkulima ina maana kuu tatu : 1.Mtazamo wako unapokuwa sawa,utagundua kwamba unatembea kwenye mafungu makubwa makubwa ya almasi yaani fursa (opportunity) ziko chini ya miguu yetu hivyo hatuhitaji kwenda popote kinachotakiwa ni ugundua nafasi hizo,unaweza ukafa ujaziona almasi hizo kinaweza kikawa kipaji kila mtu amezaliwa nacho tatizo ni kugundua kipaji hicho.

2.Majani ya upande wa pili {shamba la mwenzako} siku zote huonekana ni ya kijani zaidi kuliko ya shamba lako,wakati unaposifia uzuri wa majani ya upande wa watu wengine ujue kuna watu wengi wanayakubali majani yaliyopo upande wako na wanatamani hata kufaya kazi na wewe.Lakini kwasababu hauzingatii majani ya shamba lako unachukua muda mwingi kuangalia majani ya shamba la mwenzako hivyo unaweza kufa masikini usipokuwa makini.

Maana ya tatu 3.Bahati haiji mara mbili kwenye maisha inayofuata inaweza ikawa nzuri zaidi au mbaya,lakini kamwe haiwezi kujirudia tambua hilo watu wengi wanashindwa kutamua bahati zao na fursa hata itakapobisha hodi ama kuonyesha dalili,hata zinapotokea watu wengine huchukulia kuwa ni jambo la kawaida linapodumu wa muda na kutoweka ndipo wanagundua kuwa ilikuwa ni bahati ama fursa kama aliitumia vibaya anaanza kujuta.Maneno mabaya katika maisha ni "ningejua" tatizo hapa ni kukosa mtizamo.

No comments:

Post a Comment